Ruka kwenda maudhui

Wema Na Ubaya

MEMA na MABAYA haiko. Kitu iko muzuri kama inatufaa, na mbaya kama haitufai. MEMA na MABAYA ni mambo ya faida za ubinafsi na mawazo ya akili.

Muntu yenye alibuni maneno ya hatari MEMA na MABAYA alikuwa Atlante mwenye aliitwa MAKARI KRONVERNKZYON, muumini wa maana wa Shirika la Kisayansi AKALDAN, yenye ilikuwa ku bara yenye ilizama Atlantida.

Hajawahi kushtukia ule mutu mukubwa mwenye hekima ya zamani uharibifu mukubwa yenye ataleta kwa wanadamu, na uvumbuzi wa maneno yake mbili.

Watu wenye hekima wa Atlante walisoma sana nguvu zote za EVOLUTIVAS, INVOLUTIVAS na NEUTRAS ZA ASILI, lakini ule mutu mukubwa mwenye hekima alipata mawazo ya kufafanua zile mbili za kwanza na maneno MEMA NA MABAYA. Aliiita nguvu za aina ya EVOLUTIVO kuwa muzuri na nguvu za aina ya INVOLUTTVO alizibatiza na neno mbaya. Hakupea nguvu zisizo na upande jina lolote.

Nguvu hizo zinafanyika ndani ya muntu na ndani ya asili, nguvu isiyo na upande ikiwa ni mahali pa kutegemea na usawa.

Miaka mingi kisha kuzama kwa ATLANTIDA na POISEDONIS yake ya sifa yenye Platon anaizungumuza juu yake ku Jamhuri yake, kulikuwa ku ustaarabu wa mashariki TIKLYAMISHAYANA muhani mukubwa sana mwenye alifanya kosa kubwa sana ya kutumia vibaya maneno MEMA na MABAYA akitumia kwa ulegevu ili kujenga juu yao maadili. Jina la ule muhani lilikuwa ARMANATOORA.

Na mabadiliko ya historia kupitia karne nyingi zisizohesabika, wanadamu waliharibika na maneno haya mbili na kuyafanya kuwa msingi wa kanuni zao zote za maadili. Leo maneno haya mbili mutu anayapata hata ku supu.

Siku hizi kuna WATENDAJI wengi WA MABADILIKO wenye wanataka UPYA WA MAADILI lakini kwa bahati mbaya yao na ya dunia hii yenye inateseka akili yao imefungwa kati ya MEMA na MABAYA.

Maadili yote yanajengwa juu ya maneno MEMA na MABAYA, ndio maana kila MTENDAJI WA MABADILIKO YA MAADILI kwa kweli ni MTU WA KURUDISHA MAMBO NYUMA.

Maneno MEMA na MABAYA yanatumika sikuzote ili KUHESABISHA au KULAUMU makosa yetu wenyewe.

Mwenye anahesabisha au analaumu haelewi. Ni jambo la akili kuelewa maendeleo ya nguvu za EVOLUTIVAS lakini si jambo la akili kuyahesabisha na neno ZURI. Ni jambo la akili kuelewa michakato ya nguvu za involutivas lakini inakuwa upumbavu kuilaumu na neno MBAYA.

Nguvu yote ya kuondoka inaweza kuwa nguvu ya kukaribia. Nguvu yote ya involutiva inaweza kubadilika kuwa EVOLUTIVA.

Ndani ya michakato isiyo na mwisho ya nishati ku hali ya EVOLUTIVO kuna michakato isiyo na mwisho ya nishati ku hali ya INVOLUTIVO.

Ndani ya kila binadamu kuna aina tofauti za nishati zenye EVOLUCIONAN, INVOLUCIONAN na zinabadilika bila kukoma.

Kuhesabisha aina fulani ya nishati na kulaumu ingine, haimaanishi kuelewa. Jambo la maana ni kuelewa.

Uzoefu wa KWELI imekuwa nadra sana kati ya wanadamu kwa sababu ya kufungwa ku akili. Watu wamefungwa kati ya kinyume MEMA na MABAYA.

SAIKOLOJIA YA MABADILIKO ya HARAKATI YA GNÓSTICO inajengwa juu ya usomaji wa aina tofauti za nishati zenye zinafanya kazi ndani ya mwili wa binadamu na ndani ya asili.

HARAKATI YA GNÓSTICO iko na ETHICA YA MABADILIKO yenye haina uhusiano wowote na maadili ya watu wa kurudisha mambo nyuma wala na maneno ya kihafidhina na ya kurudisha nyuma ya MEMA na MABAYA.

Ndani ya maabara ya Kisaikolojia-Fiziolojia ya mwili wa binadamu kuna nguvu za evolutivas, involutivas na neutras zenye zinapaswa kusomwa na kueleweka sana.

Neno MEMA linazuia UELEWA wa nishati za EVOLUTIVAS kwa sababu ya kuhesabisha.

Neno MABAYA linazuia uelewa wa nguvu za INVOLUTIVAS kwa sababu ya kulaumu.

Kuhesabisha au kulaumu haimaanishi kuelewa. Mwenye anataka kumaliza kasoro zake hapaswi kuhesabisha wala kuzilaumu. Ni lazima KUELEWA makosa yetu.

Kuelewa HASIRA ku ngazi zote za akili ni jambo la maana ili ndani yetu izaliwe utulivu na upole.

Kuelewa tofauti zisizo na mwisho za tamaa ni jambo la lazima ili ndani yetu izaliwe upendo wa watu na kujitolea.

Kuelewa tamaa ya mwili ku ngazi zote za akili ni sharti ya lazima ili ndani yetu izaliwe usafi wa kweli.

Kuelewa wivu ku maeneo yote ya akili inatosha ili izaliwe ndani yetu maana ya ushirikiano na furaha kwa ustawi na maendeleo ya wengine.

Kuelewa kiburi ku matofali na ngazi zake zote ni msingi ili izaliwe ndani yetu ku njia ya asili na rahisi ua la kigeni la unyenyekevu.

Kuelewa nini ile kitu ya ulegevu yenye inaitwa uvivu, haiko tu ku namna zake za ajabu lakini pia ku namna zake za hila zaidi, ni jambo la lazima ili izaliwe ndani yetu maana ya shughuli.

Kuelewa namna tofauti za ULAFI na ulafi mwingi kunalingana na kuharibu tabia mbaya za kituo cha silika kama vile karamu, ulevi, uwindaji, kula nyama, uoga wa kifo, tamaa ya kuendeleza MIMI, hofu ya kuangamizwa, nk.

Walimu wa shule, vyuo na vyuo vikuu wanashauri wanafunzi wao wa kike na wa kiume wajiboreshe kama vile MIMI inaweza kujiboresha, wapate fadhila fulani kama vile MIMI inaweza kupata fadhila, nk.

Ni lazima kuelewa kwamba MIMI haijiboresha kamwe, kwamba haiko kamili zaidi na kwamba mwenye anatamani fadhila anaongeza nguvu MIMI.

UKAMILIFU KAMILI unazaliwa tu ndani yetu na kufutwa kwa MIMI. Fadhila zinazaliwa ndani yetu ku njia ya asili na rahisi wakati tunaelewa kasoro zetu za kisaikolojia haiko tu ku ngazi ya akili lakini pia ku maeneo yote ya akili ya chini ya fahamu na isiyo na fahamu.

Kutaka kujiboresha ni upumbavu, kutamani utakatifu ni wivu, kutamani fadhila kunamaanisha kuongeza nguvu MIMI na sumu ya tamaa.

Tunahitaji kifo kamili cha MIMI haiko tu ku ngazi ya akili lakini pia ku kila kona, mikoa, maeneo na njia za akili. Wakati, tumekufa kabisa, inabakia tu ndani yetu ILE yenye IKO KAMILI. ILE yenye imejaa fadhila, ILE yenye ni KIINI cha UTU wetu WA NDANI, ILE yenye haitokani na wakati.

Ni kwa kuelewa tu sana michakato yote isiyo na mwisho ya nguvu za evolutivas zenye zinaendelea ndani yetu wenyewe hapa na sasa. Ni kwa kuelewa tu ku njia kamili namna tofauti za nguvu za INVOLUTIVAS zenye zinafanyika ndani yetu wenyewe kila wakati, tunaweza kufuta MIMI.

Maneno MEMA na MABAYA yanatumika ili KUHESABISHA na KULAUMU lakini haiko kabisa ili kuelewa.

Kila kasoro iko na matofali mengi, asili, nyuma na kina. Kuelewa kasoro ku ngazi ya akili haimaanishi kuwa umeielewa ku maeneo tofauti ya akili ya chini ya fahamu, isiyo na fahamu na chini ya fahamu.

Kasoro yoyote inaweza kutoweka ku ngazi ya akili na kuendelea ku maeneo mengine ya akili.

HASIRA inajificha na vazi la Jaji. Wengi wanatamani kutokuwa na tamaa, kuna wenye hawana tamaa ya pesa lakini wanatamani nguvu za Kisaikolojia, fadhila, mapenzi furaha hapa ao kisha kifo, nk., nk., nk.

Wanaume na wanawake wengi wanasisimuka na wanavutika kwa watu wa jinsia tofauti “ETI” kwa sababu wanapenda uzuri, akili yao ya chini ya fahamu inawasahau, TAMAA YA MWILI inajificha na maana ya urembo.

Watu wengi wenye wivu wanawaonea wivu watakatifu na wanafanya toba na wanajichapa kwa sababu wanataka pia kufika kuwa WATAKATIFU.

Watu wengi wenye wivu wanawaonea wivu wale wenye wanajitolea kwa wanadamu na basi wakitaka kuwa wakubwa pia, wanawafanyia dhihaka wale wenye wanawaonea wivu na wanawarushia mate yao yote ya kashfa.

Kuna wenye wanajivunia nafasi, pesa, umaarufu na heshima na kuna wenye wanajivunia hali yao ya unyenyekevu.

Diogene alijivunia pipa yenye alikuwa analala ndani yake na wakati alifika ku nyumba ya Socrate alisema: “Nakanyaga kiburi chako Socrate, nakanyaga kiburi chako”. “Ndiyo, Diogene, na kiburi chako unakanyaga kiburi changu”. Ilikuwa jibu ya Socrate.

Wanawake wenye majivuno wanafunga nywele, wanavaa na wanajipamba na kila kitu chenye wanaweza ili kuamsha wivu ya wanawake wengine, lakini Majivuno pia inajificha na kanzu ya unyenyekevu.

Hadithi inasema kwamba Aristipe mwanafalsafa Mgiriki akitaka kuonyesha dunia yote hekima yake na unyenyekevu wake alivaa kanzu ya zamani sana na yenye imejaa mashimo, alishika ku mkono wake wa kulia fimbo ya Falsafa na akaenda ku barabara za Atene. Wakati Socrate alimuona akikuja, alisema: “Unaonekana majivuno yako kupitia mashimo ya mavazi yako, ewe Aristipe”.

Wengi wako ku umaskini kwa sababu ya ulegevu, lakini kuna watu wenye wanafanya kazi sana ili kujipatia maisha lakini wanahisi ulegevu wa kusoma na kujijua ili kufuta MIMI.

Wako wengi wenye wameacha ULAFI na Ulafi Mwingi lakini kwa bahati mbaya wanalewa na wanaenda kuwinda.

Kila kasoro ni ya pande nyingi na inaendelea na inafanyika ku njia ya hatua kwa hatua kutoka ngazi ya chini zaidi ya ngazi ya Kisaikolojia hadi ngazi ya juu zaidi.

Ndani ya mdundo tamu wa mstari, pia uhalifu unafichwa.

Uhalifu pia unavaa Santu, Mártir, safi, Mtume, nk.

MEMA na MABAYA haiko, maneno hayo yanatumika tu ili kutafuta kuepuka na kukwepa usomaji mkuu na wa kina wa kasoro zetu wenyewe.