Ruka kwenda maudhui

La Paz

Amani HAIWEZI kuja kupitia AKILI sababu haiko ya Akili. Amani ni ile manukato ya kupendeza ya MOYO ULIO TULIA.

Amani haiko mambo ya mipango, polisi ya kimataifa, UN. OEA, mikataba ya kimataifa ao majeshi ya kuingia yenye kupigania jina ya, AMANI.

Kama tunataka kabisa AMANI ya kweli tunapaswa kujifunza kuishi kama muangalizi wakati wa vita, siku zote tuko macho na tunalinda, na Akili ya haraka na ya kutumika, sababu AMANI haiko mambo ya MAWAZO ya kimapenzi ao mambo ya ndoto nzuri.

Kama hatujifunzi kuishi katika hali ya kuwa macho kila wakati, basi njia yenye inaongoza kuenda kwenye AMANI inakuwa ngumu, finyu na kisha inakuwa ngumu sana, itaishia mwishowe kwenye njia yenye haiko na kutoka.

Ni lazima kuelewa, ni haraka kujua kama AMANI ya kweli ya MOYO ULIO TULIA haiko nyumba yenye tunaweza kufika na iko pale msichana mrembo anatungojea kwa furaha. Amani haiko lengo, nafasi, nk.

Kufuatia AMANI, kuitafuta, kufanya mipango juu yake, kupigania jina yake, kufanya propaganda juu yake, kuanzisha mashirika ya kufanya kazi kwa ajili yake, nk., ni ujinga kabisa sababu AMANI haiko ya Akili, AMANI ni manukato ya ajabu ya moyo ulio tulia.

Amani hainunuliwe wala haiuzwe wala haiwezi kufikiwa na mfumo ya KUTULIZA, udhibiti maalum, polisi, nk..

Katika inchi zingine jeshi ya inchi inazunguka katika mashamba kuharibu vijiji, kuua watu na kupiga risasi watu wenye wanadhaniwa kuwa majambazi, hii yote ati kwa jina ya AMANI. Matokeo ya mwenendo kama huo ni kuongezeka ya UKATILI.

Ukatili unazaa ukatili mwingi, chuki inazaa chuki mwingi. AMANI haiwezi kushindwa, AMANI haiwezi kuwa matokeo ya ukatili. AMANI inakuja tu kwetu wakati tunamaliza MIMI, wakati tunaharibu ndani yetu wenyewe mambo yote YA KISAICOLOGIA yenye inazaa vita.

Kama tunataka AMANI tunapaswa kutazama, tunapaswa kujifunza, tunapaswa kuona, picha yote na sio tu kona moja yake.

AMANI inazaliwa ndani yetu wakati tumebadilika kabisa katika njia ya ndani.

Mambo ya udhibiti, mashirika YA AMANI, kutuliza, nk., ni maelezo ya pekee, pointi, katika bahari ya maisha, vipande vya pekee vya picha yote ya KUWEPO, yenye haziwezi kamwe kutatua tatizo ya AMANI katika njia yake ya msingi, yote na ya mwisho.

Tunapaswa kuangalia picha katika njia yake yote, tatizo ya dunia ni tatizo ya mtu; kama MTU hana AMANI ndani yake, jamii, dunia itaishi katika vita kwa lazima.

Wa»alimu na walimu wa kike wa shule, vyuo, vyuo vikuu wanapaswa kufanya kazi kwa ajili ya AMANI, isipokuwa kama wanapenda UKATILI na UKATILI.

Ni haraka, ni lazima kuonyesha wanafunzi na wanafunzi wa kike wa kizazi kipya njia ya kufuata, njia ya ndani yenye inaweza kutuongoza kwa usahihi kamili kwa AMANI ya kweli ya moyo ulio tulia.

Watu hawajui kuelewa kweli kile AMANI ya kweli ya ndani ni na wanataka tu hakuna mtu aingilie njia yao, wasisumbuliwe, wasiudhiwe, hata kama wanajichukulia wao wenyewe kwa hatari yao wenyewe haki ya kusumbua na kuudhi na kuchukiza maisha ya watu wenzi yao.

Watu hawajawahi kupata AMANI ya kweli na wako tu nayo mawazo ya upumbavu juu yake, mawazo ya kimapenzi, mawazo yenye hayako sawa.

Kwa wezi AMANI itakuwa furaha ya kuweza kuiba bila kuadhibiwa bila polisi kuingilia njia yao. Kwa wasafirishaji haramu AMANI itakuwa kuweza kuingiza biashara yao haramu kila mahali bila mamlaka kuwazuia. Kwa wenye wanalazimisha watu kuwa na njaa AMANI itakuwa kuuza bei ghali, kuwanyonya kulia na kushoto bila wakaguzi rasmi wa serikali kuwakataza. Kwa makahaba AMANI, itakuwa kufurahia katika vitanda vyao vya raha na kuwanyonya wanaume wote kwa uhuru bila mamlaka ya afya ao ya polisi kuingilia chochote katika maisha yao.

Kila mtu anajiundia katika akili mawazo elfu hamsini ya upumbavu juu ya AMANI. Kila mtu anadai kuinua karibu naye ukuta ya ubinafsi ya mawazo ya uongo, imani, maoni na mawazo ya upumbavu juu ya kile AMANI ni.

Kila mtu anataka AMANI kwa njia yake, kulingana na tamaa zake, ladha zake, tabia zake, desturi mbaya, nk. Kila mtu anataka kujifungia ndani ya ukuta ya ulinzi, ya ajabu, kwa kusudi la kuishi AMANI yake mwenyewe, iliyoeleweka vibaya.

Watu wanapigania AMANI, wanaipenda, wanaitemea, lakini hawajui kitu AMANI ni. Watu wanataka tu wasisumbuliwe, kuweza kufanya kila mtu mambo yake ya uovu kwa utulivu sana na kwa uhuru. Hiyo ndio wanaita AMANI.

Haijalishi mambo gani ya uovu watu wanafanya, kila mtu anaamini kama kile anafanya ni kizuri. Watu wanapata uhalali hata kwa uhalifu mbaya zaidi. Kama mlevi iko na huzuni anakunywa sababu iko na huzuni. Kama mlevi iko na furaha anakunywa sababu iko na furaha. Mlevi siku zote analeta sababu ya zambi ya pombe. Hivyo ndivyo watu wote wako, kwa kila uhalifu wanapata uhalali, hakuna mtu anajiona kuwa mwovu, wote wanajiona kuwa wenye haki na waaminifu.

Kuna wavagabondi wengi wenye wanadhani vibaya kama AMANI ni kuweza kuishi bila kufanya kazi, kwa utulivu sana na bila nguvu yoyote katika dunia iliyojaa mawazo ya kimapenzi ya ajabu.

Juu ya AMANI kuna mamilioni ya maoni na mawazo yenye hayako sawa. Katika dunia hii yenye inaumiza yenye tunaishi: kila mtu anatafuta AMANI yake ya ajabu, amani ya maoni yake. Watu wanataka kuona katika dunia amani ya ndoto zao, aina yao maalum ya amani, hata kama ndani yao wenyewe kila mtu anabeba ndani yake mambo ya kisaikolojia yenye yanazaa vita, uadui, matatizo ya kila aina.

Kwa nyakati hizi za mgogoro wa dunia kila mutu mwenye anataka kujulikana anazindua mashirika YA AMANI, anafanya propaganda na anakuwa bingwa wa AMANI. Hatupaswi kusahau kama wanasiasa wengi werevu wameshinda tuzo ya NOBEL ya AMANI hata kama wako na makaburi yote na kwamba katika njia moja ao ingine wameamuru kuua kwa siri watu wengi, wakati wamejiona katika hatari ya kufunikwa.

Pia kuna walimu wa kweli wa ubinadamu wenye wanajitoa muhanga kufundisha katika nafasi zote za dunia Mafundisho ya Kumaliza MIMI. Wale walimu wanajua kupitia uzoefu wao wenyewe kama tu kumaliza Mefistófeles yenye tunabeba ndani, ndio inatuletea sisi amani ya moyo.

Wakati chuki, tamaa, wivu, gere, roho ya kupata, tamaa, hasira, kiburi, nk. nk. zinaendelea kuwepo ndani ya kila mtu, kutakuwa na vita kwa lazima.

Tunawajua watu wengi katika dunia wenye wanajiona kama wamepata AMANI. Wakati tumewasoma kabisa wale watu, tumeweza kuonyesha kama hawajui hata kidogo AMANI na kwamba wamejifungia tu ndani ya tabia fulani ya upweke na ya kufariji, ao ndani ya imani maalum, nk., lakini kweli watu hao hawajapata hata kidogo kile AMANI ya kweli ya moyo ulio tulia ni. Kweli watu hao maskini wamejiundia tu amani ya bandia yenye katika ujinga wao wanachanganya na AMANI YA KWELI YA MOYO.

Ni upumbavu kutafuta AMANI ndani ya kuta za makosa ya ubaguzi wetu, imani, mawazo ya awali, tamaa, tabia, nk.

Wakati ndani ya Akili mambo ya kisaikolojia yenye yanazaa uadui, migogoro, matatizo, vita, zinaendelea kuwepo, hakutakuwa na AMANI ya kweli.

AMANI ya kweli inatoka kwa uzuri halali ulioeleweka kwa hekima.

Uzuri wa moyo ulio tulia unatoa manukato ya kupendeza ya AMANI ya kweli ya ndani.

Ni haraka kuelewa uzuri wa urafiki na manukato ya adabu.

Ni haraka kuelewa uzuri wa lugha. Ni lazima maneno yetu yabeba ndani yao wenyewe vitu vya uaminifu. Hatupaswi kutumia kamwe maneno yasiyokuwa na mdundo, yasiyokuwa na maelewano, machafu, ya upumbavu.

Kila neno linapaswa kuwa sinfonia ya kweli, kila sentensi inapaswa kuwa imejaa uzuri wa kiroho. Ni mbaya sana kuongea wakati tunapaswa kunyamaza, na kunyamaza wakati tunapaswa kuongea. Kuna kimya cha uhalifu na kuna maneno ya aibu.

Kuna wakati kuongea ni uhalifu, kuna wakati kunyamaza pia ni uhalifu ingine. Mtu anapaswa kuongea wakati anapaswa kuongea na kunyamaza wakati anapaswa kunyamaza.

Tusicheze na neno sababu liko na jukumu nzito.

Kila neno linapaswa kupimwa kabla ya kutamkwa sababu kila neno linaweza kuzalisha katika dunia mambo mengi ya muhimu na mambo mengi ya bure, faida nyingi ao madhara mengi.

Tunapaswa kulinda ishara zetu, tabia zetu, mavazi yetu na matendo ya kila aina. Ishara zetu, mavazi yetu, njia yetu ya kuketi kwenye meza, njia ya kuishi wakati tunakula, njia ya kuwahudumia watu katika sebule, katika ofisi, katika barabara, nk. siku zote zimejaa uzuri na maelewano.

Ni lazima kuelewa uzuri wa wema, kuhisi uzuri wa muziki mzuri, kupenda uzuri wa sanaa ya ubunifu, kuboresha njia yetu ya kufikiria, kuhisi na kutenda.

Uzuri wa hali ya juu unaweza tu kuzaliwa ndani yetu wakati MIMI imekufa katika njia ya msingi, yote na ya mwisho.

Sisi tuko wabaya, wa kutisha, wa kuchukiza wakati tunaendelea kuwa na MIMI YA KISAICOLOGIA ndani na iko hai vizuri. Uzuri katika njia yake yote hauwezekani ndani yetu wakati MIMI ILIYO VINGI inaendelea kuwepo.

Kama tunataka. AMANI ya kweli tunapaswa kupunguza MIMI kuwa vumbi ya ulimwengu. Hivyo tu ndio kutakuwa na uzuri wa ndani ndani yetu. Kutoka kwa uzuri huo itazaliwa ndani yetu uzuri wa upendo na AMANI ya kweli ya moyo

AMANI YA KUUMBA inaleta utaratibu ndani yako mwenyewe, inaondoa machafuko na inatujaza na furaha halali.

Ni lazima kujua kama akili haiwezi kuelewa kile AMANI ya kweli ni. Ni haraka kuelewa kama amani ya moyo ulio tulia haitufikii kupitia nguvu, ao kwa sababu ya kuwa wa jamii fulani ao shirika lililojitolea kufanya propaganda ya AMANI.

Amani ya kweli inakuja kwetu katika njia ya asili kabisa na rahisi wakati tunapata tena hatia katika akili na katika moyo, wakati tunakuwa kama watoto laini na wazuri, wenye wanahisi kila kitu kizuri kama kila kitu kibaya, kila kitu kizuri kama kila kitu kibaya, kila kitu kitamu kama kila kitu kichungu.

Ni lazima kupata tena utoto uliopotea, katika akili na katika moyo.

AMANI ni kitu kikubwa, kilichoenea, kisicho na mwisho, sio kitu kilichoundwa na akili haiwezi kuwa matokeo ya kapriki wala bidhaa ya wazo. Amani ni dutu ya atomiki yenye iko zaidi ya mema na mabaya, dutu yenye iko zaidi ya maadili yote, dutu yenye inatoka katika kina cha ABSOLUTO yenyewe.