Ruka kwenda maudhui

Utangulizi

“Elimu ya Msingi” ni sayansi yenye inatupatia uwezo wa kujua uhusiano wetu na wanadamu, na asili, na vitu vyote. Kupitia hii sayansi tunajua vile akili inafanya kazi, sababu akili ndio chombo ya elimu na tunapaswa kujifunza kutumia hiyo chombo, yenye ndio msingi ya utu wa kisaikolojia.

Katika hii kazi tunafundishwa karibu kwa njia ya kweli vile ya kuwaza, kupitia uchunguzi, uchambuzi, uelewa na kutafakari.

Inatuarifu, vile ya kuboresha kumbukumbu ya akili kwa kutumia vitu tatu: mtu, kitu na mahali; kumbukumbu inaendeshwa na hamu, kwa hivyo tunapaswa kuweka hamu kwa kile tunasoma ili iandikwe katika kumbukumbu. Kumbukumbu inaboresha kupitia mchakato ya mabadiliko ya alkemia yenye wanafunzi watajua kidogo kidogo wenye wanataka kuboresha maisha yao binafsi.

Kwa watu wa magharibi masomo inaanzia na miaka 6 ao ni wakati wanadhaniwa kuwa na akili; kwa watu wa mashariki, zaidi sana Wahindi, elimu inaanzia tangu mimba; kwa Wagnostiki kutoka kwa mapenzi, ni kusema, kabla ya mimba.

Elimu ya baadaye itajumuisha sehemu mbili: moja inasimamiwa na wazazi na nyingine inasimamiwa na walimu. Elimu ya baadaye itawaweka wanafunzi katika elimu ya Mungu ya kujifunza kuwa baba na mama. Mwanamke anachohitaji ni ulinzi, usalama, ndio maana msichana anajiunga zaidi na baba akiwa msichana kwa sababu anamwona kuwa na nguvu na ujasiri zaidi; mvulana anahitaji upendo, uangalizi, kumbembeleza, ndio maana mvulana anajiunga zaidi na mama kwa silika ya asili. Baadaye, wakati akili za wote wawili zinaharibiwa, mwanamke anatafuta mume mzuri ao pia mwanaume mwenye anampenda, wakati yeye ndiye anapaswa kutoa upendo, na, mwanaume anatafuta mwanamke mwenye mali ya kuishi ao mwenye kazi; kwa wengine wanapendelea uso na umbo la mwili kwa akili zao.

Inashangaza kuona vitabu vya shule, kila kazi na maelfu ya maswali, yenye mwandishi anajibu kwa maandishi ili wanafunzi wajifunze kwa akili, akili isiyoaminika ndio mahali pa kuhifadhi elimu yenye vijana wanasoma kwa bidii, hiyo elimu ya kimwili kabisa inawafanya waweze kujipatia riziki wakati wanamaliza masomo, lakini hawajui chochote kuhusu maisha ambayo wataishi, wanaingia humo wakiwa vipofu, hata hawakufundishwa kuzaa kwa njia tukufu, hiyo mafundisho inasimamiwa na wahalifu katika kivuli cha uchafu.

Inahitajika kijana aelewe kuwa mbegu yenye mwili wa binadamu unatoa, ndio kitu ya muhimu sana kwa maisha ya mwanadamu (aina), ni ya baraka na kwa hivyo matumizi mabaya yake itaharibu uzao wake. Katika madhabahu ya Kanisa Katoliki, hostia inahifadhiwa katika tabenakulo kwa heshima kubwa kama inawakilisha mwili wa Kristo, hiyo sura Takatifu; imeundwa na mbegu ya ngano. Kwenye madhabahu hai, ao ni mwili wetu, mbegu yetu inachukua nafasi ya hostia takatifu ya Ukristo yenye inafuata Kristo wa kihistoria; katika mbegu yetu tunahifadhi Kristo katika uhalisia wale tunafuata Kristo hai mwenye anaishi na kupiga katika kina ya mbegu yetu.

Tunaona kwa hamu kubwa kuwa wataalamu wa kilimo wenye wanasimamia elimu ya mimea yenye inatumikia mwanadamu, wanafundisha wakulima kuheshimu mbegu yenye wananyunyizia katika mashamba, tunaona kuwa wameboresha ubora wa mbegu ili kutoa mazao bora, wakihifadhi katika silo kubwa akiba ya nafaka, ili mbegu zenye walizalisha kwa bidii zisipotee. Tunaona vile madaktari wa mifugo, wenye wanasimamia maisha ya wanyama, wamefanikiwa kuzalisha wazalishaji ao mafahali wenye gharama yao ni kubwa mara mia kuliko bidhaa ya nyama, jambo yenye inaonyesha kuwa ni mbegu wanatoa, ndio sababu ya gharama kubwa hivyo. Ni dawa tu ya serikali, yenye inasimamia aina ya binadamu, haituambii chochote kuhusu kuboresha mbegu; tunasikitika sana kwa ucheleweshaji huu na tunaarifu wasomaji wetu kuwa mbegu ya binadamu ni rahisi zaidi kuboresha, kwa kutumia daima vyakula vitatu vya msingi: kupitia kile tunawaza, kile tunavuta na kile tunakula. Kama tunawaza tu mambo ya uongo, mambo ya kipuuzi, bila umuhimu, ndio vile mbegu tunazalisha itakuwa sababu mawazo ndio ya muhimu kwa uzalishaji huo. Kijana mwenye anasoma anatofautiana na mwenye hapati elimu katika sura na muonekano, kuna mabadiliko katika utu; Ukweli wa kuvuta bia zilizomeng’enywa katika baa na vilabu vya pombe, inaamua maisha ya wateja wenye wanaenda mara kwa mara katika hizo mahali: Watu wenye wanakula keki, nguruwe, bia, pilipili, pombe na vyakula vya kusisimua, wanaishi maisha ya tamaa yenye inawaongoza kwa uasherati.

Kila mnyama mwasherati ni mchafu: punda, nguruwe, mbuzi na hata ndege wa kufugwa licha ya kuwa ndege, kama jogoo wa nyumbani. Ni rahisi kuona tofauti yenye iko kati ya waasherati na wale mwanadamu anawafanya wasiwe na hamu ya ngono kwa nguvu ili kuwanyonya, angalia korodani za farasi wa mbio na zile za farasi wa kubeba mizigo, kati ya ng’ombe wa mapigano na mafahali wenye wanatoka kila siku katika magazeti, nguruwe mkuu ao nguruwe mzaaji, hata katika wanyama wadogo kama panya mwenye ana tamaa sana na kila mara muonekano wake ni mbaya, kitu ile ile inatokea kwa mwanaume mwasherati mwenye anaficha uchafu wake na dawa za kunukia vizuri na manukato. Wakati mwanaume anakuwa safi, mtakatifu na mwenye utakatifu, katika mawazo, maneno na matendo, anapata tena utoto uliopotea, anapendeza katika mwili na roho na mwili wake hautoi uchafu.

Vile elimu ya kabla ya kuzaliwa inafanyika? Hii inatokea kati ya wanandoa wenye wanafuata usafi, ni kusema, hawapotezi kamwe mbegu yao katika uzembe na raha ya muda mfupi, vile: Waume na wake wanataka kutoa mwili kwa kiumbe kipya, wanakubaliana na wanaomba Mbingu waongozwe kwa tukio ya kurutubisha, kisha katika tabia ya upendo ya kudumu wanaishi pamoja kwa furaha na sherehe, wanatumia wakati ambapo asili inatoa zaidi, kama vile wakulima wanafanya ili kupanda, wanatumia mchakato ya mabadiliko ya alkemia wakiungana kama mume na mke, jambo yenye inaruhusu kutoroka kwa mbegu ya kiume yenye nguvu, iliyoboreshwa na mazoea yaliyojulikana hapo awali na tukio ya mimba ya Mungu inafanikiwa kupitia njia hii, mara tu mwanamke anapogundua kuwa ana mimba, anajitenga na mwanaume, ni kusema, maisha ya ndoa inaisha, hii inapaswa kufanywa kwa urahisi na mwanaume safi kwa sababu amejazwa neema na nguvu zisizo za kibinadamu, kwa kila njia anamfanya mke wake afurahie maisha ili yeye asifikirie usumbufu wala mambo kama hayo kwa sababu yote yanaathiri fetasi yenye inaendelea, kama hii inasababisha madhara ambayo haitakuwa kukutana yenye kwa njia ya tamaa watu wanafanya wenye hawajapokea ushauri wowote katika mwelekeo huu? Jambo yenye inatoa sababu ya watoto wengi kuhisi tamaa mbaya tangu umri mdogo na kuwafanya mama zao wawe na aibu kwa njia ya kashfa.

Mama anajua kuwa anamupatia maisha kiumbe kipya mwenye anahifadhi katika Hekalu lake Hai, kama kito cha thamani, akimupatia kwa sala na mawazo yake sura nzuri zenye zitainua kiumbe kipya, kisha tukio ya kuzaliwa inakuja bila maumivu; kwa njia rahisi na ya kawaida kwa utukufu wa wazazi wake. Wanandoa wanafuata chakula yenye kwa kawaida ni siku arobaini hadi tumbo la uzazi lililotumika kama chumba cha mtoto mchanga linarudi mahali pake, mwanaume anajua kuwa mwanamke mwenye analea mtoto anapaswa kumbembeleza na kumwangalia, kwa kumupapasa kwa afya sababu aina yoyote ya tamaa ya nguvu inaathiri matiti ya mama na inaleta kuziba katika mifereji ambamo maji ya thamani yanatiririka yenye itamupatia maisha, mtoto wa tumbo lake, mwanamke mwenye anataka kufanya hii mafundisho atatambua kuwa aibu ya lazima ya kufanya upasuaji wa matiti kwa sababu ya kuziba kwa kudumu inatoweka. Ambapo kuna usafi kuna upendo na utiifu, watoto wanakua kwa njia ya kawaida na kila baya linatoweka, hivyo ndivyo elimu hii ya msingi inaanza kwa maandalizi ya utu wa kiumbe kipya mwenye tayari ataenda shuleni akiwa na uwezo wa kufuata elimu yenye itamruhusu kuishi na baadaye kujipatia peke yake mkate wa kila siku.

Katika miaka 7 ya kwanza mtoto anaumba utu wake mwenyewe kwa hivyo ni muhimu kama miezi ya mimba na kile kinatarajiwa kutoka kwa kiumbe kilicholetwa katika hali kama hizo ni jambo ambalo wanadamu hawashuku hata kidogo. Akili ni sifa ya Kiumbe, tunapaswa kumjua Kiumbe.

Mimi siwezi kujua Ukweli sababu Ukweli hauhusiani na wakati na Mimi ndio.

Hofu na woga zinaharibu hatua ya bure. Hatua ni ya uumbaji, woga ni wa uharibifu.

Kwa kuchambua kila kitu na kutafakari, tunaamsha fahamu iliyolala.

Ukweli ni kile kisichojulikana kutoka wakati hadi wakati, hauna uhusiano wowote na kile mtu anaamini au haamini; ukweli ni swali ya kujaribu, kuishi, kuelewa.

JULIO MEDINA VIZCAÍNO S. S. S.