Ruka kwenda maudhui

Mukombo Grial

Kombe Takatifu ing’aa mu usiku ya mbali ya miaka yote. Askari wa zamani ya Ulaya mu wakati ya vita ya msalaba walitafuta bure Kombe Takatifu mu inchi Takatifu lakini hawakupata.

Wakati Abraham Nabii alikuwa anarudi kutoka vita ya kupigana na wafalme ya Sodoma na Gomorra, wanasema alikutana na Melquisedec, Jini ya Inchi. Hakika mutu huyo Mkubwa alikuwa anaishi mu ngome yenye ilikuwa mujengwa kabisa pale palikuwa mujengwa Yerusalemu, muji wenye Manabii wanapenda sana.

Hadisi ya miaka mingi inasema, na hii inajulikana na watu wa mbinguni na wa dunia, kwamba Abraham alifanya Upako Gnostique na kugawana mkate na divai mbele ya Melquisedec.

Haisi vibaya kusema kama wakati hiyo Abraham alitoa Melquisedec fungu ya kumi na matunda ya kwanza kama vile imeandikwa mu Kitabu ya Sheria.

Abraham alipokea Kombe Takatifu kutoka mikono ya Melquisedec; baadaye sana, kombe hiyo ilienda kuishia mu hekalu ya Yerusalemu.

Hakuna mashaka kama Malkia wa Saba alisaidia ili jambo hili itokee. Yeye alijitokeza mbele ya Salomo Mfalme na Kombe Takatifu na kisha kumupima sana alimupatia hazina hiyo ya bei kubwa.

Yesu Mukubwa alikunywa mu kombe hiyo mu ibada takatifu ya Mwisho ya Meza kama vile imeandikwa mu Injili Ine.

Yosefu wa Arimatea alijaza Kikombe na damu yenye ilikuwa inatoka mu majeraha ya Ule anapendwa sana pale Mulima ya Vichwa.

Wakati polisi ya Roma ilivamia makao ya Senateri huyo, haikupata hazina hii ya bei kubwa.

Senateri ya Roma haikuficha tu hazina hiyo ya bei kubwa, lakini pia, pamoja nayo aliweka chini ya inchi mkuki ya Longinus yenye askari ya Roma alitumia kuchoma ubavu ya Bwana.

Yosefu wa Arimatea alifungwa mu gereza ya kutisha juu hakutaka kutoa Kombe Takatifu.

Wakati Senateri huyo alitoka mu gereza, aliondoka kuenda Roma na Kombe Takatifu.

Wakati alifika Roma, Yosefu wa Arimatea alipata mateso ya Nero juu ya Wakristo na alienda pembeni ya Bahari ya Mediteranea.

Usiku moja mu ndoto malaika alimutokea na kumwambia: “Kikombe hii iko na nguvu kubwa juu ndani yake iko damu ya Mukombozi ya Dunia.” Yosefu wa Arimatea alitii maagizo ya malaika na alifukia kikombe hiyo mu hekalu yenye ilikuwa Montserrat, Catalonia, Uhispania.

Baada ya muda, kikombe hiyo ilifanyika isionekane pamoja na hekalu na sehemu ya mulima.

Kombe Takatifu ni chombo ya Hermes, kikombe ya Salomo, chombo ya bei kubwa ya mahekalu yote ya siri.

Mu Sanduku ya Agano, Kombe Takatifu haikukosekana hata kidogo mu namna ya kikombe au gomor, ndani yake ilikuwa imewekwa mana ya jangwa.

Kombe Takatifu inaeleza kwa nguvu YONI ya mwanamuke, ndani ya kikombe hii takatifu iko utamu ya kutokufa, Soma ya watu wenye wako na mambo ya siri, kinywaji ya juu ya Mungu Watakatifu.

Kristo Mwekundu anakunywa kutoka Kombe Takatifu mu saa ya juu ya Ukristo, vile imeandikwa mu Injili ya Bwana.

Kombe Takatifu haikosekane hata kidogo pale madhabahu ya hekalu. Ni wazi, Kuhani anapaswa kunywa divai ya mwangaza mu Kombe Takatifu.

Ingakuwa upumbavu kuwazia hekalu ya siri ndani yake kikombe ya baraka ya miaka yote inakosekana.

Hii inatukumbusha Ginebra Malkia wa Majini ule alimwagilia Lanzarote divai mu vikombe vya furaha ya SUFRA na ya MANTI.

Miungu yenye haikufa inakula na kinywaji yenye iko ndani ya Kombe Takatifu; wale wenye wanachukia Kombe ya Baraka, wanatukana roho takatifu.

Mutu-Kubwa anapaswa kula na utamu ya kutokufa yenye iko ndani ya kikombe ya kiungu ya hekalu.

Kubadilisha nguvu ya kuumba ni jambo ya lazima wakati tunataka kunywa mu Chombo Takatifu.

Kristo Mwekundu sikuzote anafanya mabadiliko, sikuzote anapinga, sikuzote ni shujaa, sikuzote anashinda, anakunywa kwa ajili ya Miungu kwa kunywa mu kikombe ya zahabu.

Inueni vizuri kikombe yenu na muangalie musimwage hata tone moja ya divai ya bei kubwa.

Mukumbuke kama neno yetu ya uongozi ni THELEMA (mapenzi).

Kutoka chini ya kikombe -picha ya mfano ya sehemu ya siri ya mwanamuke-, moto zinatoka zenye zinaangaza mu uso ya Mutu-Kubwa yenye inawaka.

Miungu yenye haisemekani ya galaksi zote sikuzote inakunywa na kinywaji ya kutokufa mu kikombe ya milele.

Baridi ya mwezi inaleta mabadiliko ya kurudi nyuma mu wakati; ni lazima kunywa divai takatifu ya mwangaza mu chombo takatifu ya Alquimia.

Zambarau ya wafalme watakatifu, taji ya kifalme na zahabu ya moto ni tu kwa ajili ya Kristo Mwekundu.

Bwana ya Radi na ya Ngurumo anashika Kombe Takatifu mu mukono yake ya kuume na anakunywa divai ya zahabu ili akule.

Wale wenye wanamwanga Chombo ya Hermes mu wakati wa tendo ya ndoa ya kikemia, kwa kweli wanageuka viumbe vya chini ya mutu ya ulimwengu ya chini.

Mambo yote yenye tumeandika hapa inapatikana mu kitabu yangu yenye inaitwa “Ndoa Kamilifu”.