Ruka kwenda maudhui

Mimi Ya Akili

Hii swali ya mimi mwenyewe, nani mimi, ile kitu inafikiria, inasikia na inatenda, ni kitu tunapaswa kujitafutia ili kujua ndani kabisa.

Kuko pote pote mafundisho mzuri sana yenye inavutia na kushangaza; lakini haitasaidia chochote kama hatujijui wenyewe.

Inavutia kusoma astronomia au kujiburudisha kidogo kwa kusoma vitabu vizito, lakini inakuwa ya ajabu kuwa msomi na usijue chochote juu yako mwenyewe, juu ya mimi niko, juu ya utu wa kibinadamu tunao.

Kila mutu iko huru sana kufikiria vile anataka na akili ya akili ya mnyama anayeitwa mutu kimakosa inatosha kwa kila kitu, anaweza kufanya chawa kuwa farasi na farasi kuwa chawa; wako wasomi wengi wanaishi wakicheza na akili ya kibinadamu. Na mwisho wa yote nini?

Kuwa msomi haimaanishe kuwa na hekima. Wajinga wenye wanaonekana kuwa wanajua mambo mengi wamejaa kama magugu na hawajui tu, lakini pia hawajui kama hawajui.

Elewa kwa wajinga wenye wanaonekana kuwa wanajua mambo mengi, wale wanajiona wajanja ambao wanaamini kuwa wanajua na hawajijui wenyewe.

Tunaweza kutoa mawazo mazuri juu ya mimi wa Saikolojia, lakini sio hiyo haswa inatuvutia katika sura hii.

Tunahitaji kujijua wenyewe kupitia njia ya moja kwa moja bila mchakato wa kuhuzunisha wa uchaguzi.

Hii haitawezekana kwa njia yoyote kama hatujichunguzi wenyewe katika tendo kila wakati, kila dakika.

Sio swali la kujiona kupitia nadharia fulani au uvumi rahisi wa akili.

Kujiona moja kwa moja vile tulivyo ndio jambo la kuvutia; ni hivyo tu tunaweza kufika kwenye ujuzi wa kweli juu yetu wenyewe.

Ingawa inaonekana ya kushangaza, tumekosea juu yetu wenyewe.

Vitu vingi tunavyoamini hatuna, tunavyo na vingi tunavyoamini tunavyo, hatuna.

Tumeunda mawazo ya uwongo juu yetu wenyewe na tunapaswa kufanya orodha ili kujua kile tunacho kupita kiasi na kile tunachokosa.

Tunafikiria kuwa tunazo sifa fulani ambazo hatuna kweli na fadhila nyingi ambazo tunazo hakika hatuzijui.

Sisi ni watu tumelala, hatuna akili na hilo ndilo jambo kubwa. Kwa bahati mbaya tunafikiria mambo mazuri juu yetu wenyewe na hatushuku hata kidogo kama tumelala.

Maandiko matakatifu yanasisitiza juu ya umuhimu wa kuamka, lakini hayaelezi mfumo wa kufikia uamsho huo.

Mbaya zaidi ni kwamba wako wengi wamesoma maandiko matakatifu na hawaelewi hata kama wamelala.

Kila mtu anaamini anajijua mwenyewe na hawashuku hata kidogo kama kuna “fundisho la wengi”.

Kwa kweli mimi wa kisaikolojia wa kila mtu ni mwingi, anakuwa kila wakati kama wengi.

Kwa hili tunamaanisha kuwa tunao mimi wengi na sio mmoja tu kama wanavyofikiria kila wakati wajinga wenye wanaonekana kuwa wanajua mambo mengi.

Kukana fundisho la wengi ni kujifanya mjinga, kwa sababu kwa kweli itakuwa kilele cha kilele kupuuza ukinzani wa ndani ambao kila mmoja wetu anao.

Nitaenda kusoma gazeti, anasema mimi wa akili; kuzimu na usomaji kama huo, anasema mimi wa harakati; napendelea kwenda kutembea kwa baiskeli. Kutembea gani wala mkate moto gani, anapiga kelele mtu wa tatu katika ugomvi; napendelea kula, nina njaa.

Kama tungeweza kujiona katika kioo cha mwili mzima, vile tulivyo, tungevumbua sisi wenyewe moja kwa moja fundisho la wengi.

Utu wa kibinadamu ni kama kibaraka kinachodhibitiwa na nyuzi zisizoonekana.

Mimi ambaye leo anaapa upendo wa milele kwa Gnosis, baadaye anachukuliwa nafasi na mimi mwingine ambaye hana uhusiano wowote na kiapo; basi mtu huyo anaondoka.

Mimi ambaye leo anaapa upendo wa milele kwa mwanamke baadaye anachukuliwa nafasi na mwingine ambaye hana uhusiano wowote na kiapo hicho, basi mtu huyo anaangukia katika upendo na mwingine na jumba la kadi linaanguka chini. Mnyama anayeitwa mtu kimakosa ni kama nyumba iliyojaa watu wengi.

Hakuna utaratibu wala makubaliano yoyote kati ya mimi wengi, wote wanagombana na wanashindania ubwana. Wakati mmoja wao anapata udhibiti wa vituo vikuu vya mashine ya kikaboni, anajisikia pekee, bwana, lakini mwishowe anaondolewa.

Tukifikiria mambo kutoka kwa mtazamo huu, tunafikia hitimisho la kimantiki kwamba mnyama wa akili hana hisia ya kweli ya uwajibikaji wa maadili.

Bila shaka kile mashine inasema au inafanya kwa wakati fulani, inategemea tu aina ya mimi ambayo inaidhibiti wakati huo.

Wanasema Yesu wa Nazareti alitoa kutoka kwa mwili wa Maria Magdalena pepo saba, mimi saba, mfano hai wa dhambi saba za mauti.

Ni wazi kila mmoja wa pepo hawa saba ni kichwa cha jeshi, kwa hivyo tunapaswa kuweka kama matokeo kwamba Kristo wa ndani aliweza kufukuza kutoka kwa mwili wa Magdalena maelfu ya mimi.

Tukitafakari mambo haya yote tunaweza kuhitimisha wazi kwamba kitu pekee cha heshima tunachomiliki ndani yetu ni ESENCE, kwa bahati mbaya inapatikana imefungwa kati ya mimi hao wengi wa Saikolojia ya mapinduzi.

Inasikitisha kwamba esence inachakatwa kila wakati kwa sababu ya kufungwa kwake.

Bila shaka esence au ufahamu ambayo ni kitu kimoja, inalala usingizi mzito.