Ruka kwenda maudhui

Dawa Za Kulevya

Kujigawa kifikolojia ya mutu inatupa nafasi ya kuonyesha uhalisia mukali wa kiwango cha juu zaidi ndani ya kila mumoja wetu.

Wakati mutu ameweza kuthibitisha mwenyewe moja kwa moja ukweli kamili wa watu wawili ndani ya mutu mumoja, wa chini katika kiwango cha kawaida, wa juu katika oktave ya juu zaidi, basi kila kitu kinabadilika na tunajaribu katika hali hii kutenda katika maisha kulingana na kanuni za msingi ambazo ziko ndani kabisa ya UMUTU wake.

Kama vile kuna maisha ya nje, vile vile pia kuna maisha ya ndani.

Mutu wa inje siyo kila kitu, kujigawa kifikolojia kunatufundisha uhalisia wa mutu wa ndani.

Mutu wa inje ana namna yake ya kuwa, ni kitu na mitindo na majibu mingi ya kawaida katika maisha, kibaraka anayechezeshwa na kamba zisizoonekana.

Mutu wa ndani ni UMUTU wa kweli, unajifanyika katika sheria zingine tofauti sana, hauwezi kubadilishwa kuwa roboti.

Mutu wa inje hawezi kushona bila kidole cha kushonea, anahisi kwamba amelipwa vibaya, anajihurumia, anajiona kuwa muhimu sana, kama ni askari anatamani kuwa jenerali, kama ni mfanyakazi wa kiwanda analalamika wakati hapandishwi cheo, anataka sifa zake zitambuliwe ipasavyo, nk.

Hakuna mutu anayeweza kufika kwenye kuzaliwa kwa PILI, kuzaliwa upya kama vile Injili ya Bwana inavyosema, wakati anaendelea kuishi na saikolojia ya mutu wa chini wa kawaida.

Wakati mutu anatambua ubatili wake mwenyewe na umaskini wa ndani, wakati ana ujasiri wa kuchunguza maisha yake, bila shaka anakuja kujua mwenyewe kwamba kwa vyovyote vile hana sifa za aina yoyote.

“Heri walio maskini wa roho kwa maana wao wataupokea ufalme wa mbinguni.”

Maskini wa roho au wahitaji wa roho, ni kweli wale wanaotambua ubatili wao wenyewe, aibu na umaskini wa ndani. Aina hiyo ya viumbe bila shaka wanapokea nuru.

“Ni rahisi ngamia kupita katika tundu la sindano, kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa mbinguni.”

Ni wazi kwamba akili iliyorutubishwa na sifa nyingi, vyeo na medali, sifa za kipekee za kijamii na nadharia ngumu za kitaaluma, siyo maskini wa roho na kwa hivyo haiwezi kuingia katika ufalme wa mbinguni.

Ili kuingia katika Ufalme, hazina ya imani inakuwa muhimu sana. Wakati kujigawa kifikolojia hakujatokea katika kila mumoja wetu, IMANI inakuwa kitu zaidi ya kisichowezekana.

IMANI ni ujuzi safi, hekima ya majaribio ya moja kwa moja.

IMANI siku zote ilichanganywa na imani za bure, Wanostiki hatupaswi kuanguka kamwe katika kosa kubwa kama hilo.

IMANI ni uzoefu wa moja kwa moja wa kilicho halisi; uzoefu mzuri wa mutu wa ndani; utambuzi wa kimungu wa kweli.

Mutu wa ndani, anapojua kwa uzoefu wa moja kwa moja wa kimistikia ulimwengu wake wa ndani, ni wazi kwamba pia anajua ulimwengu wa ndani wa watu wote wanaoishi kwenye uso wa dunia.

Hakuna mutu anayeweza kujua ulimwengu wa ndani wa sayari Dunia, wa mfumo wa jua na wa galaksi tunamoishi, kama hajajua ulimwengu wake wa ndani. Hii ni sawa na mutu anayejiua ambaye anakimbia maisha kwa kupitia mlango wa uongo.

Ufahamu wa ziada wa mutu anayetumia dawa za kulevya una mizizi yake maalum katika chombo kinachochukiza cha KUNDARTIGUADOR (nyoka mshawishi wa Edeni).

Ufahamu uliomo ndani ya vitu vingi vinavyounda Ego unajifanyika kwa sababu ya kufungwa kwake.

Ufahamu wa ego unakuwa basi, katika hali ya kukosa fahamu, na ndoto za hypnotic zinazofanana sana na zile za mutu yeyote ambaye yuko chini ya ushawishi wa dawa fulani.

Tunaweza kuweka swali hili kwa njia ifuatayo: ndoto za ufahamu wa ego ni sawa na ndoto zinazosababishwa na dawa za kulevya.

Ni wazi kwamba aina hizi mbili za ndoto zina sababu zao za asili katika chombo kinachochukiza cha KUNDARTIGUADOR. (Ona sura ya XVI ya kitabu hiki).

Bila shaka dawa za kulevya zinaangamiza miale ya alfa, basi bila shaka uhusiano wa ndani kati ya akili na ubongo unakuja kupotea; hii kwa kweli inasababisha kushindwa kabisa.

Mutu anayetumia dawa za kulevya anabadilisha tabia hiyo kuwa dini na kwa uongo anafikiria kujaribu kilicho halisi chini ya ushawishi wa dawa za kulevya, akipuuza kwamba ufahamu wa ziada unaosababishwa na bangi, L.S.D., morfini, uyoga wa hallucinogenic, cocaine, heroine, hashishi, vidonge vya kutuliza akili kupita kiasi, amfetamini, barbiturate, nk, nk, nk, ni ndoto tu zilizotengenezwa na chombo kinachochukiza cha KUNDARTIGUADOR.

Watu wanaotumia dawa za kulevya wanapobadilika, wanaharibika kwa muda, wanaishia kuzama kabisa ndani ya ulimwengu wa kuzimu.