Ruka kwenda maudhui

Kazi ya Esoteriki ya Kinostiki

Ni lazima sana kusoma Gnosis na kutumia mawazo ya kimatendo yenye tunatoa mu kitabu hili ili kufanya kazi kabisa juu ya sisi wenyewe.

Lakini, hatutaweza kufanya kazi juu ya sisi wenyewe na nia ya kuvunja “Mimi” fulani bila kuangalia kwanza.

Kuona sisi wenyewe kunafanya nuru iingie ndani yetu.

“Mimi” yoyote inajidhihirisha mu kichwa kwa njia moja, mu moyo kwa njia ingine, na mu sehemu ya siri kwa njia ingine.

Tunahitaji kuangalia “Mimi” yenye tunapata imeshikwa, ni lazima kuiona mu kila kituo kati ya hizi tatu za mwili yetu.

Katika uhusiano na watu wengine, kama tuko macho na tunachunga kama mlinzi wakati wa vita, tunajigundua wenyewe.

Unakumbuka saa ngapi kiburi yako iliumizwa? Jeuri yako? Ni nini ilikukasirisha sana siku ile? Sababu gani ilikukasirisha? Ni sababu gani iliyofichwa? Soma hii, angalia kichwa yako, moyo yako na sehemu yako ya siri…

Maisha ya kawaida ni shule ya ajabu; mu uhusiano tunaweza kugundua zile “Mimi” zenye tunabeba ndani yetu.

Jambo lolote la kukasirisha, tukio lolote, linaweza kutuongoza kupitia kujitazama sisi wenyewe, kugundua “Mimi,” iwe ni ya kujipenda, wivu, hasira, tamaa, mashaka, kashfa, uasherati, nk., nk., nk.

Tunahitaji kujijua sisi wenyewe mbele ya kuwajua wengine. Ni lazima tujifunze kuona mawazo ya wengine.

Kama tunajiweka mahali pa wengine, tunagundua kama makosa ya kiakili yenye tunawapatia wengine, tunayo mengi ndani yetu.

Kumpenda jirani ni muhimu, lakini mtu hawezi kupenda wengine kama hajajifunza kujiweka mu nafasi ya mutu ingine mu kazi ya kiroho.

Ukatili utaendelea kuwepo juu ya uso ya dunia, wakati hatujajifunza kujiweka mahali pa wengine.

Lakini kama mutu hana ujasiri ya kujiona mwenyewe, anaweza kujiweka namna gani mahali pa wengine?

Sababu gani tunapaswa kuona tu upande mbaya wa watu wengine?

Kukataa mutu bila sababu yenye tunakutana naye mara ya kwanza, inaonyesha hatujui kujiweka mahali pa jirani, hatumpendi jirani, akili yetu imelala sana.

Mutu fulani hatupendi sana? Sababu gani? Labda anakunywa? Tujiangalie wenyewe… Tuko na uhakika wa wema wetu? Tuko na uhakika hatubebi ndani yetu “Mimi” ya ulevi?

Ni vizuri kama tunamuona mlevi anafanya mambo ya kipumbavu tuseme: “Huyu ni mimi, nafanya mambo ya kipumbavu.”

Wewe ni mwanamke mwaminifu na mwenye fadhila na ndiyo maana humupendi mwanamke fulani; unamchukia. Sababu gani? Unajiona salama sana? Unaamini kama ndani yako hauna “Mimi” ya uasherati? Unafikiria kama yule mwanamke aliyedhalilishwa na kashfa zake na tamaa zake mbaya ni mpotovu? Una uhakika kama ndani yako hauna tamaa mbaya na upotovu yenye unaona mu yule mwanamke?

Ni vizuri kama unajitazama wewe mwenyewe na kama mu kutafakari kirefu unaweka nafasi yako mu nafasi ya yule mwanamke unayemchukia.

Ni lazima sana kuthamini kazi ya kiroho ya Gnostic, ni muhimu kuielewa na kuithamini kama kweli tunatamani mabadiliko ya kweli.

Inakuwa lazima kujua kupenda watu wenzetu, kusoma Gnosis na kupeleka mafundisho haya kwa watu wote, la sivyo tutaanguka mu ubinafsi.

Kama mutu anajishughulisha na kazi ya kiroho juu yake mwenyewe, lakini hapeani mafundisho kwa wengine, maendeleo yake ya ndani inakuwa ngumu sana kwa kukosa kumpenda jirani.

“Mwenye anatoa, anapokea na kadri anavyotoa, ndivyo atapokea zaidi, lakini mwenye hatoi kitu hata kile alicho nacho atanyang’anywa.” Hiyo ndiyo Sheria.